ZLATAN IBRAHIMOVIC KWENDA MAN U HIVI KARIBUNI...
Usiku wa June 9 taarifa za staa wa zamani wa klabu ya Paris Saint Germain ya Ufaransa Zlatan Ibrahimovich kuhusishwa kujiunga na klabu ya Man United zimechukua sura mpya, Zlatan anaripotiwa kukamilisha hatua ya nne ya kujiunga na klabu ya Manchester United.
Dalili inayotajwa kuwa staa huyo yupo
mbioni au katika hatua za mwisho kujiunga na klabu ya Man United
zinazidi kudhihirika, baada ya kuripotiwa tayari ametafutiwa nyumba ya
kuishi katika jiji la Manchester ambapo ndio makao makuu au mji inapotoka klabu ya Man United.